Thursday 15 May 2014

UTAMJUAJE MTU MWENYE KUTAKA MAFANIKIO KATIKA BIASHARA/MRADI WAKE?


BIASHARA/MIRADI


Mwezeshaji: Pr Lupakisyo M.Mwakasweswe



JE UNAMFAHAMU WALT DISNEY?

Walt Disney: Walt alifukuzwa kutoka jiji la Kansas ambako alikuwa anashughulika na uandishi wa habari  ambako alionekana kuwa ni mtu asiyefanya mambo kwa haraka, alionekana mlegevu asiye mbunifu  kama mtoto mdogo . Kwa sasa ni mtu maarufu,  mtengenezaji wa picha zinazotembea (motion picture ) katika ulimwengu wote amepokea tuzo  kuu sana zinazo mpatia heshima kubwa sana duniani.

UTAMJUAJE MTU MWENYE KUTAKA MAFANIKIO KATIKA BIASHARA/MRADI WAKE?

Majibu ya swali  kama yalivyo jibiwa na washiriki wa semina ya Uwakili na Ujasiliamali
katika Kanisa la Wa adventista wa Sabato Ngongongare  - Arusha Tarehe 1/4/2014

1.      Anaweka malengo katika biashara yake na namna ya kuyafikia malengo.
2.      Anajuhudi katika biashara yake hapotezi muda anawajibika kikamikifu.
3.      Anaongeza juhudi na kutumia fedha yake vizuri kwanza Mungu.
4.      Anapokea ushauri kutoka kwa watu wengine wenye mafanikio.
5.      Anatumia kauli nzuri ya kuvutia wateja wake. (Ana uso wenye tabasamu).
6.      Anatumia akili ya kujua ni wapi ataweza kufanikiwa tena.
7.      Anakuwa mtu wa maombi biashara yake.
8.      Anakuwa mdadisi kwa wengine
9.      Anaamka Asubuhi na mapema kazini.
10.  Anamshukuru Mungu kwa kidogo apatacho na kukiendeleza hakatishwi tamaa.
11.  Ni mtu mwenye kuthubutu kufanya mambo.
12.  Mjasiri na mwenye kujiamini kwakile anachofanya.
13.  Mvumilivu
14.   Mbunifu.
15.  Ni mtu anaekubali kushauriwa
16.  Mkweli
17.  Akipata wazo hulifanyia kazi mara moja.
18.  Hukubali ushauri kwa watu waliofanikiwa.
19.  Hubadilika kulingana na hali ya uchumi.
20.  Baada ya mafanikio hubuni biashara nyingine ili kuongeza kipato.
21.  Huwa nakini katika mahesabu ya kazi ili kujua faida na hasara.
22.  Atajali anachokifanya.
23.  Atambue faida na hasara katika mazingira yaliyomzunguka.
24.  Atahitaji Elimu ya ziada ili kufanikisha kazi yake. 
25.  Atakua  na ratiba ya kazi  yake atatunza .
26.  Atakua mbunifu kutokana na mazingira.
27.  Atalinda mtaji.
28.  Atajali masharti ya biashara.
29.  Awe anafahamu mahitaji ya jamii iliyomzunguka.
30.  Awe tayari kujifunza/ kutafiti toka kwa wenzake.
31.  Awe na uaminifu katika shughuli zake baina yake na Mungu pamoja wateja wake.
32.  Asiwe na muda mwafaka katika kuanza biashara yake na wala muda huo usiwe wa kubadilikabadilika.
33.  Awe na bidhaa inayokubalika katika jamii yake.
34.  Awe mwaminifu katika kulipa kodi (TRA).
35.  Awe msafi binafsi na mazingira yake yaliyomzunguka.
36.  Awe na Elimu juu ya shughuli anayotaka kuanza.
37.  a) Usiogope kuanza (kuwekeza 
38.   Udadisi/ kutafuta elimu.
39.  Ana fikra chanya.
40.   kujijali / na kujali watu
41.  Mtendaji sio maneno
42.   Mwaminifu asiwe mdanganyifu.

NYONGEZA YA MWEZESHAJI
1.      Hawapendi hasara kubwa
2.      Hupenda kubeba majukumu huona kwamba kila anachpata ni matkeo ya juhudi zake
3.      Hupenda kujua matoke ya nguvu zake
4.      Ni wabunifu wa kupanga mbinu mbalimbali za shughuli zao.
5.      Ni wavumilivu kwa matatizo yanayotokea
6.      Ni mtu wa vitendo kwa mambo wanayoyapanga
7.      Si watu wa kuridhika kwa kila ambacho wanapanga

 MFANYA BIASHARA AU MTU MWENYE MRADI ANAYEFANIKIWA;
1.      Anaanza biashara yeyemwenyewe – haajiri mtu kwanza
2.      Hupenda watu maana ndiyo wateja wake
3.      Ni watu wanaojua kuongoza
4.      Hupenda kuna shughuli aliyo ianzisha imekwisha
5.      Hufanya kazi kwa malengo
6.      Huwa na mipango
7.      Wanamaamuzi ya haraka lakini ya busara
8.      Hupenda kijitegemea
9.      Huwa hawajui iwapo biashara zao zitafanikiwa wanapenda kuwajibika
10.  Wana mawasiliano mazuri na wenzao/wateja
11.  Hupenda kubadilika na wanajiamini.


3 comments:

Unknown said...

thank you Pastor kwa kutuelimisha...ubaikiwe sana.

Unknown said...

Bigup Mkuu!

Unknown said...

Asante sana mkuu.
Wengi wetu tunakata tamaa haraka, tukijaribisha tunataka matokeo mema ya haraka,tunaridhika na ujuzi kudogo wa kazi.

Post a Comment