Pr.
Lupakisyo M.Mwakasweswe
Chaplain
- Chuo Kikuu Cha Arusha
Fungu
kuu: 1 Wakorintho 7:39 Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai,
lakini ikiwa
mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye
yote amtakaye; katika Bwana tu.
Utangulizi
Ndoa ni agizo la
Mungu, ni mpango wa Mungu tangu mwanadamu alipoumbwa katika bustani ya edeni,
haukuwa mpango wa Mungu kwamba aumbe mwanadamu ili aishi katika ulimwengu wenye
shida, Dhambi ilipoingia duniani, mpango wa Mungu wa kumwuumba mwana damu awe
mwenye furaha ukabadilika kwa jinsi mwanadamu mwenyewe alipo kubali kuasi
sheria ya Mungu, mwanadamu aliposikiliza agizo la Shetani, ulikuwa ndiyo mwanzo
wa maisha yenye huzuni.
Neno kuoa au
kuolewa ni tendo la kuanzisha uhusiano kati ya mwanamke na mwanaume. Ndoa
yaweza kuelezewa kwa maana nyingi lakini moja niliyo ichagua mwandishi wa
Lessoni ya Dini ya Mahusiano ya July 2004 uk wa 45 alisema “ Ni muunganiko wa
mwanamume na mwanamke katika njia halali “, tena mwanafalsafa Aristotle
alipuliuzwa kueleza maana ya neno rafiki alisema “ Rafiki ni roho moja ikiishi
katika miili miwili.” Kwa maana hizo tunaweza kujenga hoja yetu kwamba Mungu
alikusudia kwamba watu wanao oana ni wale ambao wanafanya mahusiano yanayo
kubalika na mbingu, tena wakiwa tayari wamejiandaa kuishi pamoja kuwa mwili
mmoja. Hilo ndilo ndoa katika Bwana tu
Asili ya Ndoa
Mwanzo 18:18 – 25 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo
mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.19 Bwana Mungu
akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani,
akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu
likawa ndilo jina lake. 20 Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na
ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia
Adamu aliyefanana naye. 21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye
akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule
ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa
Adamu. 23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama
katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika
mwanamume. 24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye
ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. 25 Nao walikuwa uchi wote
wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.
Maisha yenye huzuni
ni pamoja na kuzaa kwa uchungu, kula kwa jasho, mahusiano yasiyo sahihi kwa
wana ndoa, uchaguzi mbaya wa mwenzi nk. Katika mada hii tutazingatia athari za
kuoana na mtu asiye amini.
Mungu ndiye
anayejua ninani atakaye kuwa msaidizi wako, kwa hiyo
usisumbuke kutafuta msaidizi yoyote mpaka Mungu amekupatia. Waweza kujiuliza
anakujaje? Mungu analeta mtu kwa wakati wake, Muda ukifika na umekuwa
ukimtegemea atakupatia sawa sawa na mapenzi yake.Kuna athari kubwa
sana kukataa mwongozo wa Mungu katika kuchagua mwenzi wa maisha, wahenga
walisema “ Majuto ni mjukuu”. 1 Wakorintho 7:39 Mwanamke hufungwa maadamu
mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote
amtakaye; katika Bwana tu.
Maoni ya baadhi ya
vijana kuhusu kuolewa na kuoana na Wasio amini
·
Hakuna madhara yoyote
yakuoana na mtu asiye amini kwani ni mtu ninaye pendana naye sana.
·
Mtu asiye Msabato
anamaendeleo kuliko msabato kwa sababu wasabato wengi hawajishughulishi.
·
Ndani ya kanisa vijana
wakubwa ni wachache , wamebaki watafuta njia tu, yaani (PF)
·
Wasichana wa hapa kanisani
ni wahuni sana.
·
Mbona ni mwaaminifu kuliko
vijana wa kanisa letu?
·
Nina mfahamu siku nyingi
hawezi kuwa na tabia mbaya kivile
·
Nimepanga kumleta kanisani
tukisha oana tu, naamini ataongoka tu
·
Dini pekee haiwezi
kutufikisha mbinguni, hata vijana wa kisabato wanafanya maovu mengi kuliko
wasio wasabato.
·
Kijana wa kisabato mpaka
akuoe basi amekuonea huruma kwamba ameshakuchezea sana (ni wachafu kitabia).
·
Kwa upande na wanaume husema
kuwa wasichana walioko nje ni waaminifu kiliko wanawake wa ndani, na kwa
wanaweke husema vivyo hivyo.
·
Wanaume wa kisabato huwataka
wasichana kwa kuwachezea kwanza ndipo kaamuu kama watawaoa au lah!
Mwongozo wa kanisa (Kanuni za Kanisa)
Ndoa na Familia ni
msingi wa 23 katika mwongozo wa kanisa la Wa adventista wa Sabato uk 190.
Unasema “ Ndoa ilianzishwa na Mungu katika Edeni na kuthibitishwa na Yesu kuwa
ni muungano wa maisha yote kati ya mwanamume na mwanamke katika urafiki wa
upendo. Kwa mkristo ahadi ya ndoa ni kwa Mungu pia kama ilivyo kwa mwenzi, na
hainabudi kutolewa kati ya watu wenye imani moja tu…
Kuoa na kuolewa - Agano la kale
Kumbukumbu
la torati 7:1 – 4 Bwana, Mungu wako, atakapokutia katika
nchi uendayo kuimiliki, atakapoyang'oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti,
na Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi,
mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe; 2 wakati Bwana, Mungu wako,
atakapowatoa mbele yako, nawe utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao; 3 binti yako usimpe mwanawe mume, wala
usimtwalie mwanao mume binti yake. 4 Kwa kuwa
atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu
miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye
atakuangamiza upesi.
Kumbukumbu
laTotrati 18: 9 Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako
usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.10 Asionekane kwako mtu
ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu
atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, 11 wala mtu
alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu
awaombaye wafu. 12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni
kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako. 13 Uwe mkamilifu
kwa Bwana, Mungu wako.
Kwa mafungu hapo juu,
Mungu alipowapa nchi wana wa Israeli alitaka waishi maisha makamilifu. Mungu
alifahamu uwepo wa makabila ambayo hayakumpenda Mungu kwa sababau waligeukia
miungu mingine. Mungu alitahadharisha wazazi na watoto kwamba wasifanye maagano
nao wala wasioane nao, maana kuna kukengeushwa.
Unapoanzisha
uhusiano wa ndoa, kumbuka kwamba una mvuto mkubwa wa mahusiano ya ngono,na hi
iimefanya wengi kujikuta wameingia katika tendo la ndoa kabla ya wakati wao.
Kuwa na uhusianao na makabila yaliyo mwasi Mungu Mhiti, na
Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, mataifa
saba makubwa yenye nguvu kupita Israeli Mungu alionya wasiwe na mahusiano nao
kwa kuwaozesha wana wao. Endapo unafahamu mwenendo mbaya wa mtu Fulani na
hujaweza kumwambia ni rahisi sana ukaiga mwenendo huo.
Kuoa na kuolewa – Agano
jipya
2 Wakorintho 6:14 -18 Msifungiwe nira pamoja na
wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki
na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?15 Tena pana ulinganifu
gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye
asiyeamini? 16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa
maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa
ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu
wangu.17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu
kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu
wanangu wa kiume na wa kike.
Mtu mwingine aweza kusema, fungu hili linamaana
nyingine na siyo muungano wa ndoa. Hata kama mwandishi wa fungu hili ametaja
jambo lingine ukweli unabaki pale pale
kwamba mahusiano ya muumini na mtu asiye muumini haiwezekani labda yawe mahusiano yaliyo
katika Bwana, ndiyo yanayofaa, mahusiano
yoyote yasiyo mpendeza Mungu hayangefaa kwa mtu wa Mungu, iwe ni katika kuoa au
kuolewa au katika mahusiano ya kibiashara isiyo halali. Mungu anataka kutengana
na watu wasiomwamini.
Wengi wametumia fungu kuhalalisha kuoana na mtu
asiye amini kwa kusoma fungu la 1Wakorintho
7: 12 - 14 “Lakini watu wengine nawaambia mimi,
wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana
mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa
naye asimwache. 13 Na mwanamke, ambaye ana mume
asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye,
asimwache mumewe. 14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na
yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu
wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.”
Mwandishi
anafundisha waumini waliokutwa na injili
wakiwa tayari katika mahusiano ya mke na mume , hakukuwa na sababu ya kuachana
ila kuonyesha upendo wa Kristo kwa mwenzi wake na ili aiamini injili. Hapa
haiwezi kuwa kibali cha mtu kuoa au kuolewa na mtu asiye amini.
Ndoa ya
zaidi ya Mke Mmoja
Hebu tuangalie mazingira yamtu anaye owa
au kuolewa katika ndoa ya Zaidi ya mke mmoja; Kitabu cha Mwongozo wa Kanisa uk
214 tole la 18 sahihisho la 2010 unasema “Desturi ya kuwa na wake wengi
miongoni mwa watu wasio Wakristo tunao wahubiria injili katika makabila mengi,
hupingana na kanuni za Kikristo. Kwa hiyo Kanisa letu limeshika maelekezo
yafuatayo:
1.
Mtu akiwa na wake wengi
wakati injili inapomfikia, akibadilika moyo, basi atatakiwa kuitengeneza hali
yake kwa kuwaacha wake zake wote na kubaki na mmoja tu, kabla hajahesabiwa
kustahili ubatizo na kuingia katika ushirika wa kanisa.
2.
UK 216 namba 4 inasema “Tunatambua
na kukubali haki ya mke, aliyeachwa na mume mwenye wake wengi kuolewa tena.
3.
Uk 216 namba 5 inasema “Wake
za mtu walioolewa naye walipokuwa hawamjui Mungu, ambao baada ya kupokea imani
ya Kikristo hawawezi kuachana na mume wao kutokana na sababu na desturi za
kimila/utamaduni, wakipata kibali cha kamati ya Konferensi, au union
wanawezakubatizwa na kupokelewa katika ushirika wa kanisa . Lakini mwanamke
aliyemshiriki akiolewa kama mke wa pili au zaidi, ataondolewa katika ushirika
wa kanisa, na hatapokelewa tena katika ushirika wa kanisa
mpaka aachane na Yule mume.
Hayo ni mazingira ya watu, wanawake na wanaume walio ndani ya ndoa
na wamepata injili bada ya kuoa na kuolewa, kwa hiyo mtu asitumie mafungu ya
Biblia kuficha ukweli kuhusu mahusiano ya mke na mume.
Nabii wa Mungu Ellen G. White akiandika
katika kitabu cha Kutayarisha njia sehemu ya 1, uk 137. anasema. “ Wale wanao iungama kweli
huyakanyaga mapenzi ya Mungu kwa kuoana na
wasioamini; wanapoteza kibali cha Mungu na kufanya
kazi ngumu ya kutubu. Huenda mtu asiyeamini akawa mwenye tabia njema ya moyoni
lakini kwamba hajaungama majibu ya madai ya Mungu naye amekataa wokovu mkuu namna
hii ni sababu ya kutosha inayo acha umoja usikamilishwe. Pengine tabia ya Yule
asiye amini ikafanana na ile ya Yule kijana ambaye Yesu alimwambia maneno haya,
“Umepungukiwa na neno moja;” hilo litakuwa neno moja lenye kutakikana sana.”
Nuru kwa kanisa uk 141 Mwandishi anasema
“Kamwe watu wa Mungu wasingethubutu kuingia mahali palipokatazwa na Mungu. Ndoa
baina ya waaminio na wasio amini imekatazwa na Mungu. Lakini mara nyingi moyo
usioongoka hufuata tama zake mwenyewe, na ndoa zisizo kubaliwa na Mungu
hufanywa. Kwa sababu hii wanaume na wanawake wengi hawana tumaini wala hawanaye
Mungu ulimwenguni. Mivuto yao bora imekufa kwa mnyororo wa hali ya mambo haya
wameshikwa wavuni mwa shetani. Wale wanaotawaliwa na ashiki na tama mbaya ya
mwili watakuwa na mavuno machungu kuvuna katika maisha haya, na mwenendo wa
waweza kuleta hasara ya roho zao mwishowe.
Amosi 3:3 Je! Watu wawili
waweza kutembea
pamoja,
wasipokuwa wamepatana?. Kwa muktadha wa Biblia, watu wawili hawawezi kutembea
pamoja kama hawajapatana. Kwa watu wana mwamini Mungu hawataweza kupatana na
mtu asiye mpenda Mungu , watapatana tu kwa sababu ya kuongoa roho na sio kwa
sababu ya kuoa na kuolewa. Vijana wengi waetumia njia hii kuhalalisha ndoa za
imani tofauti kwa kusingizia kwamba wamepatana. Mungu anataka watu wake
wapatane katika mambo matakatifu.m Ndoa ni Takatifu kama ilivyo Sabato, wale
wanaoingia katika muunganik wa tendo hili ni wajibu wao kuchukua tahadhali ili
wasije wakajikuta wanafanya mapatano na mtu asiye muumini wa imani yake.
Nuru kwa kanisa uk 143 Mwandishi anasema
“ Kila Mkristo apaswa kufanya nini akiingizwa mahali pa kujaribiwa nguvu ya
imani yake?. Kwa uthabiti wenye
kustahili kuigizwa yampasa aseme dhahiri: “Mimi ni mkristo mwaminifu. Naamini
kuwa siku ya saba ya juma ni Sabato ya Biblia. Imani na kanuni zetu zimeachana,
ni tofauti hata hazipatani. Hatuwezi kufurahi pamoja, mana kama nikiendelea
kujipatia ujuzi kamili zaidi wa mapenzi ya Mungu, nitazidi kuhitilafiana na
walimwengu na kufanywa nifanane zaidi na kristo.”
Mwongozo wa Kanisa uk 170 toleo la 18
sahihisho la 2010 unasema “Kwa kawaida roho ya Unabii inashauri dhidi ya ndoa
kati ya “anayeamini na asiyeamini” na inatoa tahadhari zaidi dhidi ya kuungana
na Wakristo wenzetu ambao “hawajaupokea ukweli wa wakati huu”. – 5T 364.Inaendelea Kwa kusema “Kanisa linatambua kwamba ni haki
ya mtu binafsi kufanya uamuzi wa mwisho kuhusu uchaguzi wa mwenzi wa ndoa. Hata
hivyo, ni tumaini la Kanisa kwamba kama mshiriki atachagua mwenzi ambaye si
mshiriki wa Kanisa, wenzi hao watatambua na kuelewa kuwa Mchungaji wa kanisa la
Waadventista wa Sabato aliyeahidi kusimamia kanuni zilizelezwa hapo juu ,
hatatarajiwa kufungisha ndoa hiyo. Mshiriki akiingia katika ndoa ya aina hiyo, kanisa halina budi kuonesha upendo na kujali kwa kusudi la kuwatia moyo wanandoa hao kuingia katika umoja
kamili ndani ya Kristo.
Pamoja na hayo, katika ukursa wa 210, Mwongozo
wa Kanisa unasema, “Ndoa ya Kikristo– Kwa sababu tunakubali kwamba kanisa hupimwa
kutokana na kawaida zake za mema na mabaya, na kwamba ndoa ya Kikristo
inayokubalika na wengi inafaa kwa wakristo wa Kanisa la Waadventist wa Sabato, tunasisitiza
ushauri kuwa makanisa yetu yote yawafundishe washiriki wao kupata huduma ya
ndoa ya kisheria na kikanisa, ambapo watu wanaoona
hupatana na kuzishika kanuni zinazotawala ndoa ya Kikristo.
Inashauriwa kwamba mshiriki akioa au
kuolewa na mtu aliye katika darasa la ubatizo, apate pia huduma hiyo ya
kisheria na Kikanisa. Kama watu walio katika darasa la ubatizo wameoana kwa njia ya kimila,
basi inashauriwa wafanyiwe huduma ya kisheria
na ya Kikanisa kabla hawajabatizwa.
Adventist Home, uk 61 – 69 Mwandishi anasema “Ni
jambo la Hatari kufanya ndoa ya kidunia. Shetani ajua Sana kuwa saa ya ndoa ya
vijana wa kiume na wa kike hufunga historia ya maisha yao
ya dini na ya manufaa. Hawamo kwa kristo. Pengine kwa muda mfupi
watafanya jitihada kuishi maisha ya kikristo; lakini jitihada zao zote
zinakutana na mvuto wa nguvu unazipinga.”
Miongoni
mwa Athari za kuoana na Mtu asiye amini
Athari za kuoana na mtu asiye amini kama zinavyo andikwa na Mjumbe
wa Mungu Ellen G. White katika kitabu cha Kutayarisha Njia 1 uk 137. Anasema;
1.
Kupungua kwa hali ya mambo
ya kiroho huanzia dakika ile ya kuahidi kwa kiapo kwenye mimbara
2.
Moyo wa bidii wa mambo ya
dini unapunguzwa, na ngome moja mja huvunjwa mpaka wote wote wawili wamekuwa
hali moja chini ya bendera nyeusi ys shetani.
3.
Katika furaha ya Harusi roho
ya kidunia hushinda dhamiri, imani na kweli
4.
Katika nyumba hiyo mpya na
saa ya maombi haiheshimiwi tena. Wamejichagua wenyewe na kumfukuzia mbali Yesu.
5.
Furaha anasa za kidunia
hupendelewa sasa ili kumfurahisha mwenzi mpagani.
6.
Mwenzi hatapenda kusoma ama
kusikiliza Biblia kisha atasema: “Ulioana na mimi, ukijua kwamba nalikuwa hali
hii nilivyo sasa; sitaki kusumbuliwa”
7.
Kisha mashaka hujongea
taratibu juu ya mambo ya Mungu na hatimaye anapoteza imani
8.
Uchaguzi unafanyika sasa
aidha apote upendo kwa Mungu kabisa kisha adumishe upendo wa mwenzi wake
asiyeamini ama aupoteze kwa mwenzi kisha ndoa ipasuke.
4 comments:
nimeipenda sana hii...barikiwa sana mtu wwa Mungu!!
Barikiwa
Ubarikiwe sana Mchungaji,Endelea kuzijenga ndoa zetu na kuwaa daa vema vijana wetu.
Mungu akubariki sana pasta endelea kutubari sisi vijana
Post a Comment