Sunday 11 May 2014

MUZIKI NA UIMBAJI KATIKA IBADA




UTANGULIZI


Muasisi Mkuu wa Muziki na Uimbaji ni Mungu.  Muziki uliumbwa kwa matumizi matakatifu, kuinua mawazo kwa mambo yaliyo safi, mema na kuamusha katika moyo ibada na Shukurani kwa Mungu.”   Ellen White anaendelea kusema: “Muziki ni moja ya sanaa ya pekee.  Muziki mzuri hauleti tu burudiko la rohoni, bali pia bali huyainua akili katika vimo vya juu kwa mambo mazuri.  Mungu mara nyingi ametumia nyimbo za kiroho kugusa mioyo ya wadhambi na kuwaongoza kutubu. Kwa upande mwingine nyimbo zaweza kubomoa tabia adilifu na kututenga mbali na mahusiano   yetu na Mungu.”
Mama Ellen katika toleo hilo lililotajwa hapo juu ana haya ya ziada kuhusiana na kitengo ch a Muziki¨ Ellen G. White, Tumaini la Vizazi Vyote. Washington DC:  Review and Herald Publication Association p 73   Ibid.,  Uinjilisti wa Vitabu uk 43 Muziki waweza kuwa na mvuto mkumbwa kwa ajili ya mambo ya kupendeza, hata hivyo Hatujatumia huduma hii katika ibada kama ipasavyo. Mara nyingi nyimbo zimeimbwa   Kiholela bila mpangilio maalumu kufuatia matukio Fulani na mara nyingi wale wafanyao. Huduma hii wameachwa kufanya wapendavyo, na hivyo muziki hupoteza makusudi yake Kwa wale wanaosikiliza.  Muziki ni muhimu kuwa na Uzuri, mvuto na nguvu. Hebu sauti   Ziinuliwe kwa nyimbo za sifa na ibada. Utumiaji wa vyombo waweza kushirikishwa ili Utamu wake umfikie Muumbaji kama sadaka inayokubalika.” Ibid., uk 114
Muziki ulibuniwa na Mungui kwa ajili ya Ibada, Ukaagizwa na Mungu na , Ukabarikiwa na Mungu.  Wakati wa uumbaji nyota za asubuhi ziliimba na kwaya ya malaika wakapaza sauti zao kwa furaha.  (Ayubu 34:4-7).  Sehemu inayofuata tutaona jinsi Muziki ulivyovurugwa na adui.

HISTORIA YA ANGUKO AU UCHEPUKAJI WA VIWANGO VYA MUZIKI

VITA KUU BAINA YA KRISTO NA SHETANI

 KATIKA MUKTADHA WA MUZIKI


Vita kuu baina ya Kristo na Shetani ambayo ilianzia kule mbinguni ikafanya Lucifer MalaikaAliyekuwa kiongozi Mkuu wa Kwaya ya Malaika kule mbinguni alipotamani nafasi ya Mungu kama alivyotamka “nitakipandisha kiti changu juu kupita nyota za Mungu….nitafanana kama Mungu” Lucifa alitaka aabudiye. ( Isaya 14: 13,14 ) Mungu anataka aabudiwe na ndiyo stahili Yake kwa maana yeye ndiye muumbaji wa wote.  Shetani naye anataka aabudiwe
Na amefaulu Sana kupokea ibada ambayo haimstahili kwa kupitia kuwakilisha tabia ya Mungu vibaya kwa njia ya Muziki ambao ameuandika ili kusudi kulishinda kanisa la Mungu. Mdanganyifu mkuu akitambua ya kuwa muda wake ni mfupi sana amebuni njia hii ya kuwanasa Waadiventista Wanaodai kuwa wanamtii pamoja na kushika Sabato yake takatifu na kutunza amri kumi za Mungu kwa kupitia Muziki wa duniani ambao haumpi Mungu utukufu na Sifa badala yake humpa Ibilisi utukufu na Sifa japo unaimbiwa mbele ya kusanyiko takatifu la wasafiri wa mbinguni.
Ibilisi akitambua kuwa Ibada ndiyo njia rahisi ya kuliharibu kanisa la Mungu, amekusudia kuharibu utakatifu wa Muziki katika Ibada kuanzia katika bustani y Edeni. Vita kuu ya Muziki ambayo ilianzia katika bustani ya Edeni ni halisi, na hivyo ni muhimu kwetu kuelewa kama kanisa jinsi ambavyo uimbaji umeharibiwa leo na Yule adui, na sasa hebu na tufuatie historia ya Muziki na uchepukaji katika kanisa la Mungu la kweli.

ANGUKO LA KWANZA CHINI
YA MLIMA SINAI


Historia inaanzia na Waisrael wa Zamani (ambapo sisi tu Waisrael wa Kiroho).  Wakati walipokuwa wakisafiri baada ya Mungu kuwaokoa kutoka katika utumwa wa Misri  wakielekea katika nchi ya ahadi (Kaanani); wakati Musa alipoagizwa kukwea mlimani ili kupokea amri kumi za Mungu, watu (wakiongozwa na Kuhani Haruni) Walishangilia na kufanya ibada kwa ndama wa dhahabu, wakitoa sadaka, wakinywa na kucheza na kuimba. Muziki ambao uliambatana na Sherehe yao ulikuwa na Sauti kubwa na usio na mpangilio  kiasi ambacho Joshua alipokuwa akishuka toka mlimani pamoja na Musa wadhani ya kuwa illkuwa kelele za vita.
Lakini Musa Mtumishi wa Mungu akasema, La  hasha; ni kelele za watu wanaoimba. ( Kutoka 32:18). Jinsi watu walivyoimba na kucheza Haruni akawa akawaongoza  hata kubakia uchi wakimshangilia ndama wa dhahabu, ibada ambayo iliwaangusha katika zinaa. ( Kutoka 18:25 ).  Huu ulikuwa uasi wa Kwanza Mkuu kwa watu Wateule wa Mungu katika siku za awali kabisa za kanisa la Mungu. Muziki huu ambao ulibuniwa na Shetani ulikusudiwa kuwafanya watu kumvunjia Mungu heshima. Kama matokeo ya kumtii Yule adui na kukengeuka katika njia ya Mungu “wakaanguka watu wasiopungua elfu tatu.” (Kutoka 32:28)

ANGUKO LA PILI MASHARIKI MWA YORDANI


Takribani miaka kama arobaini (40) baada ya kuvuka bahari ya Shamu, wakati Musa Mtumishi wa Bwana alipokuwa tu amekwisha kutoa maagizo ya muhimu kabla ya kuvuka mto Yoridani ili kuingia katika nchi ya ahadi waliengesha mahema yao Baali- Peori upande wa mashariki  ufuoni mwa mto Yoridani Watu wa MUNGU kwa njia ya kujichanganya na mataifa wakaanguka katika anasa.
 Kwa mara NYINGINE TENA walishiriki katika Muziki wa mataifa na kucheza. Tendo hili likawapeleka mbali zaidi wakazama katika anasa, unywaji na ibada ya sanamu na muziki ule ukawafanya wakaanguka katika zinaa na kuanguka kiroho. Kwa njia hii Waisraeli walijiunga na ibada ya kipagani na kumuasi Mungu.  Na kwa mara nyingine tena adhabu kubwa iliwaangukia na zaidi ya watu elfu kumi waliangamizwa. Ibid. Wazee na Manabii 453-456

BAAL – PEORI YA KARNE YA LEO


Leo watu wa MUNGU kwa mara nyingine tena Waadiventista wa Sabato tupo tumepumzika katika mipaka ya Kaanani – Kaanani ya Mbinguni. Swali la Kujiuliza ni hili Je inawezekana kuona hali ile ya uasi kama ilivyokuwa katika Baal- Peori katika makanisa yetu ya sasa?  JIBU NI NDIO
Tupo katika kingo za Yordani tayari  kwa kuingia katika Kaanani ya Mbinguni ila tunachelewa hapo wakati tunangojea kumwagwa kwa Mvua ya Masika, na Kutoa kilio Kikuu cha kuutangaza ujio wa mwokozi wa haraka. Swali jingine la kujiuliza ni hili je wengi wetu makanisani hatujafanana na madhehebu mengine  hasa katika suala la ibada kwa njia y Muziki?  JIBU LA SWALI HILI PIA LAWEZA PIA KUWA NDIO.  Angalizo letu n ( 1 Yohana 2 :15)

ANGUKO NAMBA TATU ( 3 ) MARA TU BAADA YA MWAKA 1844


Baada ya tukio la Baal – Peori tunaposafiri kihistoria tunaingia wakati ambapo kanisa hili lilikuwa changa ndipo tu limeanza baada ya Mwaka 1844. Baada tu ya Mwaka 1844 wakati waumini watangulizi walipokuwa wanatazamia ujio wa Kristo kwa mara ya pili na kukosa kuja,
Kama vile inavyoweza fananishwa na Waisrael walipoanza safari yao ya kuingia katika kaanani ya duniani; watangulizi wenzetu walianza safari yao ya kuelekea katika kaanani ya mbinguni.  Katika kipindi hicho kulikuwa na hali Fulani ya utata katika historia ya Muziki wa Kiadiventista.  Ellen White anaeleza juu ya ekengeukaji uliojitokeza mnamo kipindi hicho kule Marekani. Katika sehemu nyingi Muziki wetu uliingiwa na hali ya makelele, kuruka na kucheza.  Mjumbe wa Mungu alitumwa na kusema yafuatayo: “ Nilitoa ushuhuda wangu kama onyo katika jina la Bwana nikikemea hali hii iliyojitokeza.”    Jambo la kutisha ni kuwa katika tukio hili baada tu ya mwaka 1844, watu walikaa uchi na matokeo yake yakawa kukengeuka na uovu ndio yalikuwa matokeo yake.
 Ki historia ni muhimu kuelewa ya kwamba kipindi hiki kanisa likiwa bado changa kuanzia mwaka ( 1865 – 1900 ) ndicho kipindi cha ugunduzi wa Muziki wa Jazz na Jazz ni jina linalosimama badala ya kujamiana (sexual intercourse ) ambalo lilichipuka katika nyumba za makahaba kule New Orleans, Lousiana .  Hiki ni kipindi ambacho marekani ilisumbuliwa na nyimbo hizi ambazo zilikuwa mpya na zikiwa na alama ukosefu wa adabu na kinyama pamoja na kuleta aibu.” Ibid., 2 Nyaraka Zilizochaguliwa (SM) uk 3  J. Simons.  Nyimbo za mporomoko wa Maadili, uk 35-39 
Angalizo hapa ni kuwa wakati kanisa la Mungu la kweli lilipokuwa limeanzishwa na bado changa, Mwana muziki aliyeanguka alikuwa pale tayari kuharibu utakatifu wa Muziki katika ibada ya kanisa ambalo analichukia sana.  Shetani anahitaji ibada yetu. Kwa kuanza kuandika Muziki mpotovu ambao pole pole ungelitoa kanisa katika njia yake sahihi na kuleteleza ujumbe wa malaika wa watatu.
Angalizo jingine ni kuwa Shetani ambaye ni Mwana Muziki Mkuu aliyeongoza kwaya  ya malaika watakatifu kule mbinguni, amegundua kile ambacho ana uwezo wa kukishambulia katika maisha ya mfuasi wa kristo nacho ni kutawala na ubongo wa binadamu kwani ni kwa njia hii ambayo Mungu anatumia kuwasiliana na binaadamu”
 Iwapo ubongo wa binaadamu ndio unaotawala maisha ya binaadamu hivyo basi kuna mantiki kwamba Shetani atafanya shambulizi lake la kwanza na la Mwisho kwa njia ya kutawala ubongo wa binadamu. Na iwapo Muziki ni zana ya muhimu sana katika matashi na tabia ya mwanadamu hivyo itakuwa kawaida kueleweka kuwa, Shetani atatumia Muziki kufikia malengo yake ya kumshambulia mfuasi wa kristo Ibid. uk 352

ANGUKO LA MSINGI WA MUZIKI SEHEMU YA NNE (4)
 KATIKA JIMBO LA INDIANA (MAREKANI)


Katika Konferensi ya Indiana kule Marekani mnamo mwaka 1900 lilitokea tukio jingine Ambalo lilikuwa la kutisha katika kanisa letu. Baadhi ya Makanisa yetu kule Indiana yalikuwa yakiendesha ibada zikiwa na nyimbo zenye moto wa kigeni. 
Nyimbo hizo zilisikika katika sauti kubwa , zikiwamo ngoma , sauti nzito za vyuma na ghasia zingine. Muziki tena ulio na mchanganyiko wa kishetani ulidhihirishwa katitka makanisa hayo na Roho mtakatifu kwa kawaida asinge tamalaki katika ibada kama ile alisema mjumbe wa Mungu, Ellen G. White. Kufuatia tukio hili la Indiana , Ellen G. White alitabiri ya kuwa hali hii ya Muziki uliojaa makelele na ukiwa na dalili zote za kishetani katika ibada,utaletwa tena katika kanisa la Waadiventista wa Sabato muda mfupi tu kabla ya kufungwa kwa mlango wa rehema.”Sikiliza vile mjumbe wa Mungu asemavyo kufuatia tukio lile kule Indiana: Ibid ., uk 36
“mambo uliyoelezea kutokea kule Indiana, Mungu amenionyesha kuwa Yatarudiwa tena kitambo kidogo kabla ya kufungwa kwa mlango wa rehema.  Kila aina ya vitu visivyofaa vitaachiliwa. Kutakuwepo na makelele, upigaji wa Ngoma kuimba na kucheza. Via vya kufanyia maamuzi vitapumbazwa kiasi Kwamba haviwezi kuaminiwa kufanya uamuzi ulio sahihi na hii itaitwa ni Huduma ya Roho Mtakatifu wa Mungu. Roho Mtakatifu kamwe hawezi Kujidhihirisha kwa njia hii, wala katika sauti za makele kama zile. Hizi ni    Mbinu za shetani za kutweza ukweli. Ni bora kutokuwa na muziki wa jinsi Hii wa kumsifu Mungu kuliko kutumia muziki na jinsi hii ambao mweziJanuary nilijulishwa kuwa muziki huu utaletwa katika mkutano wa Makambi. Ibid. 36

JE KUCHEZA DANSI, VITENDO NA KUMACHI NA MIHEMKO VINA MWONEKANO GANI KATIKA HUDUMA YA UIMBAJI?


Swali la msingi ni hili je kucheza wakati wa uimbaji ni sahihi? (Shall we dance?) Jiibu la swali hili laweza kutokana na kile ambacho kimekwisha onekana katika historia ya Anguko na ukengeukaji wa Muziki kuanzia Edeni, Chini ya mlima Sinai, Baal – Peori mahali Waisrael walipojenga hema hali wakijiandaa kuingia Kanani. Pia walipokuwa wakivuka Bahari ya shamu, Katika Mikutano ya Makambi kule Indiana, Baada ya mwaka 1844, na miaka ya 1990 na kuendelea ambapo imekwisha bainika kuwa Walisrael walipokengeuka  katika kujichanganya na mataifa, kushiriki katika sherehe zao, za ulafi, makelele , kuruka na kucheza kuwa adhabu yake ilikuwa kumbwa na hivyo Mungu hakupendezwa na mtindo wa jinsi hiyo wa ibada. Hivyo basi kucheza dansi hakukubaliki katika ibada takatifu.
Ni muhimu pia kupata ushauri mwingne toka kwenye Biblia juu ya suala hili. Mara nyingi kitendo cha Mfalme Daudi kinatafsiriwa visivyo.  Maandiko ni kweli yanashuhudia kwa maneno yafuatayo: “ Naye Mfalme Daudi akacheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote.”  Mfalme Daudi alicheza sio katika mazingira ya Ibada. Uchezaji wake ulifanyika nje ya ibada ndani ya hekalu, na hiyo inaleta tofauti kubwa.  Kucheza kwa Daudi kulifanyika katika mazingira ya Sherehe ya kushangilia na kushereheka moyoni kwa kuona ya kuwa hatimaye Sanduku la Agano la Bwana limerejeshwa Yerusalemu. ( 2 Sam 6:14, 16 ).
Hivyo basi hapa kuna tukio tofauti na lile ya wakati ibada inapokuwa inaendeshwa katika hekalu.  Miriam na wanawake walishika Makuyamba na wakiimba na kushangilia ukuu wa Mungu wakati alipowavusha katika bahari ya Shamu na kuwashinda Wamisri na jeshi lake walipogharakishwa ndani ya bahari ya Shamu. ((Kutoka 15:1-21)
Wanawake waliimba na kucheza wakati Daudi alipomshinda Goliath (I Sam 18:6,7 ) Binti wa Jephthah aliimba na kucheza alipokuwa anampokea baba yake wakati akitoka vitani kuwaamua waisrael toka kwa maadui zao. (Waamuzi 11:34). Hivyo twaona ya kuwa kucheza dansi kusiwe na uhusiano wakati huduma ya nyimbo inapokuwa inafanyika katika ibada takatifu.
Kufanya Vitendo, Kumachi na Mihemko vinapunguza uzito wa ujumbe ambao umetolewa katika huduma ya uimbaji kwani wasikilizaji badala ya kutafakari ujumbe unaotolewa badala yake usikivu wao unagawanyika kuangalia usanii wa mihemko ya waimbaji, au Maching au usanii wa vitendo  hivi kwa kiasi kikubwa vinahafifisha ujumbe wa mahubiri yanayotolewa na mhubiri wa Kwanza Yaani Kwaya. Hivyo ili kuongeza usikivu wa wasikilizaji ni muhimu ya kuwa wahudumu.Waruhusu ujumbe wao uende kama ulivyotolewa bila ya kuongeza vikorombezo vya vitendo vinavyofikiriwa kuwa vya muhimu. Utukufu kwa Mungu kusudi la Uimbaji
Kusudi kubwa la huduma ya uimbaji nikwa ajili ya kumtukuza Mungu. Mwimbaji anabadilishwa na wasikilizaji pia wanabadilishwa na ujumbe wanaousikia kupitia wa kwaya.  Mawazo yao, huzuni zao, Masumbuko yao, misiba yao, mikasa ya maisha vyote vinakutana na ujumbe wenye matumaini kwa Mungu ambaye kwa kumtumainia aweza kuwachukulia mizigo yao na kuwaweka huru.  Hii ndiyo sababu ni muhimu ujumbe uende kama ulivyo ili mwishoni wasikilizaji wasije wakawatukuza wahudumu kwa ajili ya matendo yanayoonekana kwa macho ya kibinaadamu badala ya kurudisha utukufu kwa Mungu.
Muziki wa kiadiventista unapaswa kuwa na tofauti na muziki unaotolewa na wahudumu wengine ambao sio waadivenstista.  Kwa vile Waadiventista ni watu wa pekee kwa kila kitu. Muziki pia unapaswa uinue bendera ya uadiventista na Kristo atukuzwe katika huduma zao.

MATUMIZI YA VYOMBO VYA MUZIKI KATIKA IBAD

Vyombo vya Muziki vyaweza kutumika katika Uimbaji iwapo mambo ya fuatayo yatatiliwa maanani:
  1.  Mpigaji wa vyombo kwa mfano Piano au Kinanda ni budi awe mtaalamu wa kutumia vyombo hivyo.
  2. Mchezaji awe na Ujuzi wa kusoma Notes na kucheza (Awe mjuzi wa Tonic so lfa na Staff Notation.
  3. Mchezaji asitumie miziki iliyoandaliwa na kuhifadhiwa katika Keyboard au Piano (Ready made Musical accompaniments) Atawale Keyboard au piano au Organ badala ya kutawaliwa na vyombo hivi.
  4. Aepuke Sana matumizi ya sauti ya juu, midundo, ambayo inatisha na kuwafanya watoto wadogo waogope.
  5. Ahakikishe kuwa sauti ya vyombo hivyo, inaruhusu maneno yasikike (lyrics) ambayo ndiyo hasa muhimu katika muziki.
  6. Awe mnyenyekevu, awe tayari kupokea mashauri asiwe na kiburi ambacho ndicho kilileta anguko la Mkurugenzi wa awali ya kwaya ya Mbinguni ambaye hatimaye alianguka kwa sababu ya kiburi chake.
  7. Afahamu jinsi ya kutawala sauti ya vyombo iende sambamba ikiacha nafasi ya maneno kusikika vema (melody, harmony rhythm na balance. ) viende sawia.
  8. Awe tayari kushirikiana na Uongozi wa Kanisa.
Angalizo: Iwapo vigezo hivyo havizingatiwi, ni bora kuimba bila kutumia vyombo vya Muziki.

MAAMUZI YA MKUTANO ULIOFANYIKA KWAKOA (NETCO) MWAKA 2003 CHINI YA IDARA YA VIJANA NA NYIMBO


Mnamo mwaka 2003 kule Kwakoa katika wilaya ya Mwanga, kamati iliyoteuliwa na kupewa majukumu ya kushughulikia maswala ya Nyimbo hasa kuhusiana na matumizi ya Vyombo vya Muziki (Accampaniments) Maamuzi yalikuwa kama ifuatavyo:
      “Watumiaji wa vyombo vya muziki hasa Vinanda ambao hawana ujuzi wa kitaalamu wa matumizi ya vyombo hivyo, Waache kutumia katika kwaya vyombo hivyo hadi watakapokuwa na wataalamu ambao wamejifunza Kusoma na Kucheza vyombo hivyo.Hivyo iliwekwa bayana kuwa kutumia vyombo vya Muziki, Kinanda, au piano ndicho kiwango kinachotakiwa.  Matumizi ya beats au midundo na mapigo vulivyopandikizwa katika Vinanda viachwe kabisa. “
      Konferensi hii chini ya uongozi wa Mchungaji Izungo wakati akiwa Mwenyekiti wa Konferensi wakati huo. Alitoa msimamo ambao ni bora ufuatwe na kitivo cha Muziki cha Kanisa.Unangalifu unahitajika kufanyika katika maeneo haya kwani hii ni sehemu dhabiti ya Msukumo wa Kanisa la Waadiventista wa Sabato ulimwenguni ulio na kauli mbiu ya “Uamsho na Matengenezo.”   John Kimbute, Mwenye kiti wa Kamati ya Muziki wa Konferensi, Kwakoa NETC, 2003.
Kwa Kuzingatia Maamuzi hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yamebadilisha na kupunguza kasi iliyokuwepo ya matumizi ya vyombo hivyo kiholela inapokuwa sio kwa makanisa yote bali yapo matengenezo ambayo ni dhahiri. Kwa kuunga mkono maamuzi hayo Samuele Bacciocchi katika kitabu chake kiitwacho: The Christian and Rock Music, anayo haya ya kusema:
      “Viongozi wa Ibada wanaosisitiza utumiaji wa vyombo kadhaa, kama vile Ngoma, Magita    yenye Sauti nzito ya Bass (Bass Guitar) na magita yenye pandikizo la kutoa muziki wa “Rock” katika makanisa yao wanapaswa waelewe ya kuwa kule Yerusalemu katika hekalu  na katika hekalu la mbinguni hakuna vyombo vya jinsi hiyo vinaruhusiwa.” Samuele Bacchiocchi et al   Tha Christian & Rock Music A Study on Biblical Principles of Music. Michigan: Bilbical Perspective,2000) P 177
      “Viongozi wa Ibada wanaoruhusu waimbaji kutumia Ngoma,Magita ya Bass na Magita     ya kuvuma sana ili kuleta sauti ya muziki wa Jazz au rock ni muhimu kwao watambue       ya kuwa katika hekalu la Bwana kule Yerusalemu na pia katika hekalu la Mbinguni.       Hapakuwa na vyombo vyenye sauti kubwa zinazotengeneza (Okestra) katika ibada. Kinyume chake vilikataliwa vyombo aina mbili na vyote vya nyuzi tu ndivyo      vilivyoruhusiwa kutumika katika ibada” Ibid Ni vema pia ieleweke kuwa hakuna kosa lolote kutumia filimbi na Matoazi. Ila vyombo Hivi havikutumiwa kwani vilikuwa vimezoeleka katika matumizi ya miziki ya duniani(Secular Music )  .
       Iwapo vyombo vya muziki vyenye sauti kali vingeruhusiwa kutumika katika ibada, ibada ingebalishwa kuwa mahali pa maburudisho. Hata wanawake Ambao walizoelea sana kucheza dansi hawakuruhusiwa kuwa sehemu ya kwaya. Daudi alichagua wanaume kuwa tu ndio waimbaji.  Hii haina maana kuwa wanawake leo wasijumuishwe katika kwaya isipokuwa iwapo wapo ambao ni wachezaji dansi katika miziki ya kidunia (dance) iwapo hao watafahamika, si vema wahusishwe katika muziki wa kumsifu Mfalme wa utukufu.  Hii ina maana kuwa wale wanaocheza miziki ya kidunia kama kazi wasingeruhusiwa kusimama mbele za mkutano wa watakatifu na kumtukuza Baba wa Utukufu. Hili ni angalizo la muhimu.

NYIMBO ZA KIHOLELA ZIMEHARIBU SURA YA MUZIKI

WA KIADIVENTISTA


  Ili kurejesha sura ya Muziki wa kiadiventista ni muhimu kwaya pamoja na vikundi vya kwaya vizingatie machache yafuatayo:-
  1. Uimbaji upangwe katika Notes  1.  Tonic  Sol fas na 2. Staff Notation
  2. Nyimbo zisiimbwe bila mpangilio kujifunza kwa muda wa kutosha ili zinapoimbwa ziwe zinasikika vizuri.(kwaya ya mfalme Daudi ilifunzwa kwa mda wa miaka mitano)
  3. Ni vema Theme za Nyimbo zetu zizingatie Ujio wa Yesu, Huduma ya Kristo katika patakatifu na Sabato ambalo ni tarajio la pumziko la milele pale Mungu atakapofanya maskani yake pamoja na Wanaadamu.
  1. Kwaya au Vikundi vya Uimbaji viwe na sare inayoelewekaKwani waimbaji  ni wahubiri.-sare ziwe mavazi ya heshima na kusitiri mwili
  2. T shirts zisitumike kama vazi la kusimama mbele ya kusanyiko la watakatifu, na kila aina ya mavazi yanayoweza kuhafifisha huduma ya ibada( isipokuwa katika matukio maalumu)
  3. Waimbishaji wawe na taaluma katika kuongoza nyimbo wafanye bidii katika kujifunza namna ya kufuata mapigo.
  4. Kwaya na Vikundi vyote viandikishwe na kupitishwa na kanisa mahaliaHebu tujifunze kwa kuangalia mfano wa kwaya za mbinguni

MFANO WA MUZIKI WA KWAYA ZA MBINGUNI


Hebu na tujifunze katika kwaya tatu zilizoko mbinguni.  Samuelle Bacchiocchi katika utafiti wake wa Theolojia ya Muziki wa Waadiventista wa Sabato anatujuza kuwa kufuatana na Utafiti wa Oscar Cullman katika kitabu cha Ufunuo kuna kwaya tatu kule mbinguni:- Kwaya ya Wazee Ishirini na Nne (24 ) Ufunuo 4:10 – 11) Mada yao kuu ni kumsifu Mungu kama Muumbaji Wakisema . Wewe Bwana ndiwe  unastahili utukufu, heshima na Uweza, na mwisho wanamsifu Mungu kwa ajili ya wale  waliokombolewa na sifa kwa mwana kondoo wa Mungu ( Wanaimba kutumia Vinubi)  harps).  Yohana anasema,” Nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi,  kama sauti ya Ngurumo ndipo nikasikia sauti toka kwa Wapiga vinubi wakipiga vinubi  vyao”( Ufunuo 14;2) Pia wanaimba wimbo mpya (Ufunuo 5:8-9) 
Malaika na Waliokombolewa ambao hesabu yao ni kubwa.  (Ufunuo 5:11-12; 7:9-12)  Mada kuu ni sawa na ile ya Wazee ishirini na Nne Kwaya ya Wote  (Mass Choir) ikihusisha viumbe wote na Waliokombolewa (Ufunuo 5:13) Wakiwa na matawi ya mitende na mavazi meupe.Mada yao kuu ni: Wokovu ni wa Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi na Mwana Kondoo.(Ufunuo 7: 9 – 10)  Wote wanaelekeza sifa na Utukufu kwa Utatu Mtakatifu.
 Kufuatana na Thomas Seel anasema kuwa Kinubi ambacho ni chombo cha nyuzi pekee kinachotumika katika kwaya za mbinguni katika ibada kimepewa kibali kwani ni rahisi kuendana (blending) na sauti za waimbaji.”  IbidYohana wa Ufunuo anatumia neno “Prokuneo” akiwa na maana ya kuwa muziki wa mwisho wa wakati ni muhimu uonyeshe heshima na kicho ili sifa zielekezwe kwa yeye ambaye anastahili,baba wa mbinguni.

HITIMISHO


Mambo makuu (5) ni ya Muhimu kuzingatiwa katika huduma ya Muziki
  1. Muziki wa Kiadiventista ni muhimu uonyeshe heshima na kicho mbele za mahali pa ibada kwani ndio wakati tunakutana na Mungu
  2. Vyombo vya kuzindikiza Muziki vichezwe na wataalamu wa kuvitumia vyombo hivyo na visisikike zaidi na kuzuia maneno ambayo ndiyo yamebeba ujumbe wa Mungu.
  3. Muziki unapotolewa uonyeshe Furaha na uchangamfu wa kuwa mbele za Mungu (Uf. 7:12)
  4. Uwiano uwepo katika Ujumbe unaotolewa na mpangano wa Sauti na ulete somo mahususi linaloweza kueleweka
  5. Waimbaji  wa Kwaya ya Kanisa na Vikundi wawe na sare kadri iwezekanavyo na mavazi ya heshima ya kujiwasilisha vizuri mbele ya watu na Mbele za Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana.
  6. Muziki na huduma ya Uimbaji katika maandiko ni sawa kama Sadaka ya Shukrani kwa Mungu, Ya Uumbaji, ulinzi wa Mungu na Wokovu wa Milele.
  7. Hebu tufanye matengenezo ya kuturejesha katika mapito ya zamani wa Muziki wa Kiadiventista. (Yeremia 6:16.)  Mungu na awabariki.






2 comments:

PR SAGUDA LUBAPULA, UNIVERSITY OF ARUSHA said...

UBARIKIWE PR, HILI SOMO NI SOMO MWAFAKA SANA

Unknown said...

Imekuwa Mbaraka mkubwa, naomba kama itakupendeza hizo nukuu hasa pale ulipoandika Ibid ingekuwa umeitaja kabisa maana ukisoma nukuu inayokuwa imetangulia kisha ukikutana na nukuu inayosema Ibid unakosa muunganiko wa hiyo nukuu hasa unapoenda katika kitabu rejea .

Unaweza kutuweka footnotes ambayo zitatuelekeza turejee vitabu gani. Zaidi nikupongeze kwa kazi njema

Post a Comment