Saturday 18 May 2013

ZABURI 23

1 Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
 2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
 3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
 5 Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
 6 Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

0 comments:

Post a Comment